0
MSANII wa filamu Bongo, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ ameshangazwa na madai kuwa, anahusika kuvunjika kwa uchumba wa msanii mwenzake Rose Ndauka na kueleza kuwa hayo ni maneno ya watu wasiomtakia mema.
NDAUKA
Akizungumza na mwandishi wetu kuhusu madai hayo, Batuli alisema hajawahi kuwa na uhusiano wowote na bwana wa Rose (Malick) na kwamba ukaribu wao ni wa kikazi tu.
Mwanadafada mkali wa Bongo Movies, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’.
Yobnesh Yusuph ‘Batuli’.

“Jamani siwezi kutoka na mchumba wa Rose kutokana na kwamba ni mtu ambaye namheshimu sana na tumekuwa tukifanya kazi na Rose bila matatizo yoyote. Hizi taarifa zinanishangaza na najua wanaozieneza hawanitakii mema,” alisema Batuli.

Post a Comment

 
Top